TAMKO LA ACT-WAZALENDO BAADA YA MKUTANO WAO KUZUIWA NA POLISI.

Baada ya Jeshi la polisi kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa Chama Cha ACT- Wazalendo kilipanga kufanya kongamao Jumapili ya June 12 2016 kwa lengo la kujadili Bajeti ya Serikali ya mwaka 2016/2017.

Taarifa iliyotolewa na chama cha ACT-Wazalendo kupitia kwa Mwenyekiti wa chama hicho Anne Mghwira imesema kwamba kongamano hilo lililenga kumpa fursa ya pekee kiongozi wa chama hicho Zitto Kabwe kusema yale ambayo angeyasema bungeni baada yeye na wabunge wenzake sita wa upinzani kusimamishwa kuhudhuria vikao vya bajeti bungeni.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa katika hali isiyo ya kawaida walipewa taarifa na mwenye ukumbi (LAPF Millenium Tower) kwamba polisi walikuwa wametanda katika eneo la ukumbi tangu saa kumi mbili asubuhi na ilipofika saa nne kamili asubuhi mwenye ukumbi aliwataarifu rasmi kuwa amepewa taarifa na kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kinondoni kwamba chama chao hakina kibali cha kufanya kongamano hilo na hivyo asiwafungulie ukumbi huo.



Hivyo kupitia taarifa hiyo chama ACT-Wazalendo kimesema kimesikitishwa sana na hatua hiyo ya polisi na wanaitafsri kuwa ni mwendelezo wa hatua za uhakika katika kufifisha demokrasia katika nchi.
TAMKO LA ACT-WAZALENDO BAADA YA MKUTANO WAO KUZUIWA NA POLISI. TAMKO LA ACT-WAZALENDO BAADA YA MKUTANO WAO KUZUIWA NA POLISI. Reviewed by Unknown on 6:54 AM Rating: 5

No comments