MARAFIKI WA ISAAC, ALIYEHUKUMIWA KWAKUMTUKANA RAIS ACHANGIWA MILIONI 4.5 YA FAIN

Marafiki wa Isaac Habakuk pamoja na wadau ambao hawakupendezwa na hukumu dhidi yake ya kwenda gerezani miaka 3 au kulipa faini ya milioni 7 kwa kudaiwa kumtukana Rais Magufuli kupitia mtandao wa Facebook kwa kutumia neno bwege wamemkabidhi jumla ya shilingi milioni 4.5 kwa ajili ya kulipa faini kuepuka kifungo gerezani.

Akikabidhi fedha hizo Jijini Arusha mchana wa leo, mwakilishi wa marafiki hao, Ndg Ephata Nanyaro amesema fedha hizo zimekusanywa kutoka kwa marafiki mbalimbali ambao wametafutana kwa njia ya simu na kila mmoja kuchangia kuanzia sh 500 na kuendelea mpaka zikafika kiasi hicho.

Fedha hizo ni makusanyo ya michango ya makundi mawili, moja likiratibiwa na Ephata Nanyaro na lingine likiratibiwa na Malisa Godilistern, wote wanachama wa Chadema na ambao hutumia mitandao ya kijamii kueleza mawazo yao kuhusu mambo mbalimbali.


Nanyaro amesema wameamua kufanya harambee ya kumchangia kijana mwenzao aepukane na dhahama ya kutotumikia kifungo kwasababu kwa jinsi sheria ya makosa ya mtandao ilivyo, kila mwananchi yuko hatarini kupelekwa gerezani kwa sheria hiyo kwasababu inavifungu ambavyo vinakiuka msingi mkuu na uhuru wa binadamu kuwaza na kujieleza.
MARAFIKI WA ISAAC, ALIYEHUKUMIWA KWAKUMTUKANA RAIS ACHANGIWA MILIONI 4.5 YA FAIN MARAFIKI WA ISAAC, ALIYEHUKUMIWA KWAKUMTUKANA RAIS ACHANGIWA MILIONI 4.5 YA FAIN Reviewed by Unknown on 7:03 AM Rating: 5

No comments